Programu ya Funguka App ni mfumo wa kidijitali unaomwezesha mtumiaji kuripoti vitendo vya ukatili kwa njia ya maandishi au sauti.

Pia, inatoa fursa ya kupata elimu ya kisheria na haki za msingi kupitia jukwaa salama linalosimamiwa na WiLDAF Tanzania.
Kazi na Faida za Funguka App
Programu hii inalenga kuleta mabadiliko chanya katika jamii kupitia vipengele vifuatavyo:

Kuripoti Ukatili:

Inatoa njia rahisi na ya siri ya kuwasilisha malalamiko ya ukatili wa kijinsia au wa aina nyinginezo. Unaweza kutoa taarifa kupitia ujumbe au kurekodi sauti.

Elimu ya Haki na Sheria:

Inajumuisha maktaba ya maarifa inayomsaidia mtumiaji kuelewa haki zake za kisheria na taratibu za kufuata pindi anapokumbana na changamoto mbalimbali.

Male Champions:

Sehemu inayotoa mwongozo na hamasa kwa ajili ya malezi bora ya watoto na ujenzi wa jamii iliyo salama.