We are excited and humbled to have the Honorable Dr. Samia Suluhu as our Guest…

Tamko Kupinga Udhalilishaji wa Viongozi Wanawake kwa njia ya Mitandao ya Kijamii
Mtandao wa Kupambana na Ukatili wa Kijinsia (MKUKI), ukiratibiwa na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF) unatoa pongezi za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa uteuzi na mabadiliko ya viongozi wa Wizara, Mikoa na Wilaya uliofanywa Jumamosi tarehe 28/07/2018. MKUKI umefarijika sana na uteuzi huo kwani umezingatia vigezo vyote muhimu ikiwemo taaluma, ueledi, uwakilishi wa makundi ya rika mbalimbali ,uzoefu na usawa wa kijinsia.
Sisi MKUKI, tumekuwa tukipigania usawa wa kijinsia katika ngazi za kutoa maamuzi ili kuleta usawa wa kijinsia baina ya wanawake na wanaume. Tunatambua jitihada za Mhe. Rais wetu katika kuhakikisha wanawake wanakuwa sehemu ya wafanya maamuzi. Katika teuzi hizo tumeona wanawake 10 wameteuliwa kuwa wakuu wa wilaya kati ya 31 na 2 wameteuliwa kuwa makatibu Tawala kati ya 13.
Kwa kipekee, MKUKI tunapenda kuwapongeza wanawake hawa malkia na vinara ambao jamii na vyombo vya uteuzi vimetambua talanta, uwezo na ujuzi wao. Tunaamini kuwa uteuzi wa uongozi umezingatia ueledi na uwezo wa kitaalamu sifa ambazo viongozi wateule wanazo. Miongoni mwao viongozi hawa wateule wameishawahi kuwa mameneja wa kampeni katika umri mdogo, wajasiriamali na tena kupewa tuzo na jarida la Forbes chini ya miaka 30 katika bara la Afrika. Watu kama hawa wamekuwa mfano wa kuigwa miongoni mwa vijana, wanawake na watoto.
Hata hivyo, MKUKI unasikitishwa na kulaani vitendo vinavyoendelea vya udhalilishaji na lugha za matusi vinavyofanywa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii hapa nchini vikilenga kudhalilisha na kudhihaki, viongozi wanawake wateule hususan Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Bi. Joketi Mwegelo. Vitendo hivyo havikubaliki kwani ni ukatili mkubwa wa kijinsia na kinyume za haki za binadamu. Vitendo hivi vinadhalilisha wanawake wote, vinaingilia uhuru wa
mtu binafsi na vinaleta chuki baina ya jamii zetu. Ikumbukwe kuwa Sheria ya Mtandao Namba 14 ya Mwaka 2015 Kifungu cha 23 (1) & (2) inakataza mtu yeyote kutumia mtandao kuonea, kutishia, kudhalilisha au kumdhoofisha kihisia na kumsababishia huzuni mtu mwingine(cyber bullying).
Tunawaasa wanajamii kutotumia vibaya mitandao ya kijamii katika kudhihaki au kumdhalilisha Mhe. Jokate na viongozi wengine wote wa serikali na taasisi binafsi. Katiba ya Jamhuri ya Muungano inampa kila mtu haki ya kutoa maoni bila kuathiri haki ya mtu mwingine. Aidha ibara ya 12-(1) na (2) inatambua heshima na thamani ya utu pamoja na usawa na haki bila ubaguzi wowote.
Tunatoa wito kwa vyombo na mamlaka husika ikiwemo Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi na kubaini wahusika ili sheria ichukue mkondo wake kukomesha vitendo vya udhalilishaji dhidi ya wanawake , hususan kwa viongozi wetu.
Tunawatakia kila la kheri wanawake wote walioteuliwa katika nafasi hizi adhimu walizozipata kuwatumikia wananchi katika kuleta maendeleo na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii, kiuchumi na kiutendaji.
Imeandaliwa na:
1 | Women in Law and Development in Africa (WiLDAF) | Dar es salaam | ||
2 | Legal and Human Rights Centre (LHRC) | Dar es salaam | ||
3 | Tanzania Gender Network Program (TGNP) | Dar es salaam | ||
4 | Tanzania Women’s Lawyers Association (TAWLA) | Dar es salaam | ||
5 | Women Legal Aid Centre (WLAC) | Dar es salaam | ||
6 | Child Dignity Forum (CDF) | Dar es salaam | ||
7 | Tanzania Media Women Association (TAMWA) | Dar es salaam | ||
8 | Tanzania Network for Legal Aids Provider (TANLAP) | Dar es salaam | ||
9 | Kivulini Women’s Rights Organization | Mwanza | ||
10 | Centre for Women and Children Assistance (CWCA) | Mara | ||
11 | Taasisi ya Haki za Wanawake (HAWA) | Dar es salaam | ||
12 | Word Vision Tanzania | Dar es Salaam | ||
13 | Kilimanjaro Women Information Exchange and Community Organization (KWIECO) | Kilimanjaro | ||
14 | Organization for Women Empowerment (OWE) | Lindi | ||
15 | Agape Foundation | Shinyanga | ||
16 | Tanzania Women and Children Welfare Centre (TWCWC) | Dar es salaam | ||
17 | Gender Centre | Dar es salaam | ||
18 | Anti-Female Genital Mutilation (AFNET) | Dodoma | ||
19 | Wanawake katika Jitihada za Kimaendeleo (WAJIKI) | Dar es salaam | ||
20 | Young Lawyers Foundation | Dar es salaam | ||
21 | Women Action Towards Economic Development (WATED) | Dar es salaam | ||
22 | Umoja wa WanawakeWanasiasa Tanzania (ULINGO) | Dar es salaam | ||
23 | Dignity Kwanza- Community Solutions | Dar es salaam | ||
24 | Chama cha Wajane Tanzania (TAWIA) | Dar es salaam | ||
25 | Women Fighting Aids in Tanzania (WOFATA) | Dar es salaam | ||
26 | Kikundi cha WanawakeWajasiriamali (ASE) | Dar es salaam | ||
27 | TLD | Dar es salaam | ||
28 | Centre against Gender Based Violence (CA-GBV) | Dar es salaam | ||
29 | Tanzania Women’s Cross Party Platform (TWCP) | Dar es salaam | ||
30 | Young Women’s Christian Association (YWCA) | Dar es salaam | ||
31 | EKAMA Foundation | Dar es salaam | ||
32 | LASEHA | Dar es salaam | ||
33 | AWWOR | Dar es salaam | ||
34 | Kigogo Youth Organization (KYO) | Dar es salaam | ||
35 | Gender Media of Southern Africa Tanzania (GEMSAT) | Dar es salaam | ||
36 | Zamzam Women Development (ZAWODE) | Dar es salaam | ||
37 | VICOBA Kigamboni | Dar es salaam | ||
38 | Network against Female Genital Mutilation (NAFGEM) | Kilimanjaro | ||
39 | National Network in Tanzania Women with HIV/AIDS (NETWO+) | Dar es salaam | ||
40 | Lindi Women’s Paralegal Aid Centre (LIWOPAC) | Dar es salaam | ||
41 | Action for Justice for Society Tanzania (AJISO) | Dar es salaam | ||
42 | New Hope New Winner’s Foundation | Dar es salaam | ||
43 | Tanzania Women of Impact Foundation (TAWIF) | Dar es salaam | ||
44 | Songea Paralegal Centre (SOPCE) | Songea | ||
45 | Wasaidizi wa KisheriaMtwara | Mtwara | ||
46 | Wasaidizi wa KisheriaTanga | Tanga | ||
47 | Wasaidizi wa KisheriaBahi (SULUNGAI) | Dodoma | ||
48 | Wasaidizi wa KisheriaKongwa (MWITAZAJE) | Dodoma | ||
49 | Wasaidizi wa KisheriaRungwe (WAKIRU) | Mbeya | ||
50 | Wasaidizi wa KisheriaKipunguni (Sauti ya Jamii) | Dar es Salaam | ||
51 | Education Centre for the Advancement of Women Tanzania | Dar es Salaam | ||
52 | Equality for Growth | Dar es Salaam | ||
53 | Women Fund Tanzania | Dar es Salaam | ||
54 | Women Wake-up (WOWAP) | Dodoma | ||
55 | Mwezeshe Mama | Dar es Salaam | ||
AHSANTE
This Post Has 0 Comments